Mamlaka Sudan yashughulikia athari za maporomoko ya ardhi

Timu za uokoaji kwa kushirikiana na wakaazi wa eneo la milima ya Jebel Marra jimbo la Darfur zinaendelea na juhudi za kuopoa miili, ingawa wanakumbwa na changamoto kubwa kutokana na ukosefu wa vifaa na ukubwa wa janga hilo. Kulingana na takwimu rasmi idadi ya watu waliopoteza maisha katika mkasa huo inakadiriwa kuwa kati ya watu 300 na 1,000. Baraza la mpito la uongozi wa kijeshi chini ya usimamizi wa Jenerali Abdel Fattah al-Burhan limeahidi kuhamisha raslimali zote zilizopo ili kusaidia waathiriwa, wakati serikali pinzani ikitangaza iko tayari kuanza juhudi za kutoa misaada.