Posts

Mazungumzo ya Marekani na Iran yaanza

Image
Wawakilishi wa Marekani leo wanatarajiwa kufanya mazungumzo na wenzao wa Iran huko Muscat, Oman kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran. Upande wa Marekani, mjumbe maalum Steve Witkoff na Jared Kushner, mkwe wa Rais Donald Trump, watashiriki. Ajenda halisi ya mkutano huo bado haijulikani. Wizara ya mambo ya nje ya Iran imesema Iran inapania kuyawekea mipaka mazungumzo hayo yajikite katika mpango wa nyuklia wa Iran na kulegezwa kwa vikwazo. Marekani ingependa kuongeza mada zaidi kwenye ajenda, ikiwa ni pamoja na mpango wa makombora wa Iran na msaada kwa washirika wake, ikiwa ni pamoja na kundi la Hamas katika Ukanda wa Gaza, wanamgambo wa Hezbollah nchini Lebanon na waasi wa Houthi nchini Yemen.

BILIONI 18 KUWASHA UMEME VITONGOJI RUVUMA

Image
Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeimarisha usimamizi wa miradi ya kusambaza umeme vitongojini mkoani Ruvuma kwa lengo la kuhakikisha vitongoji vyote nchini vinapata nishati hiyo ifikapo mwaka 2030. Wakati wa ziara ya ukaguzi mkoani humo Februari 01, 2026, Meneja wa Usimamizi wa Miradi ya REA, Mha. Deogratius Nagu, amebainisha kuwa wakala huo unakagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ili kujionea maendeleo yake halisi. Mhandisi Nagu amemuelekeza mkandarasi, kampuni ya MF Electrical Engineering Ltd, kuongeza kasi ya ujenzi wa Mradi wa Ujazilizi Fungu 2C unaohusisha wilaya za Songea, Mbinga, na Nyasa. Hadi sasa, vitongoji 88 kati ya 148 vimeshawashiwa umeme, huku mkandarasi akitakiwa kukamilisha haraka usambazaji katika vitongoji 60 vilivyosalia ili wananchi waanze kunufaika na huduma hiyo. Mradi huo unatekelezwa kwa gharama ya shilingi bilioni 18.294 na unatarajiwa kunufaisha wateja wa awali wapatao 6,781 mkoani Ruvuma. Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limesisitiza kujipanga kikamil...

Rwanda yajaribu programu inayotegemea akili bandia (AI) kuboresha huduma za afya kwa wakazi

Image
  Mradi huoI ambao unaitwa Horizon 1000, uliotengenezwa na Wakfu wa Gates na kampuni ya Marekani ya OpenAI kwa ushirikiano na mamlaka ya Rwanda, unalenga kushughulikia uhaba mkubwa wa wataalamu wa afya nchini. Ikiwa imejaribiwa kwa miaka miwili katika kliniki zipatazo hamsini za Rwanda, programu hiyo inaweza kutumwa katika vituo 1,000 vya afya kote barani Afrika ikiwa matokeo yatakuwa ya uhakika. Je, akili bandia (AI) inaweza kuboresha upatikanaji na ubora wa huduma za afya? Nchini Rwanda, Wakfu wa Gates kwa sasa unazindua programu ya majaribio ya programu mpya iliyoundwa ili kuwasaidia wataalamu wa afya katika kufanya maamuzi yao. Nchi hii inakabiliwa na uhaba mkubwa wa wafanyakazi wa afya na miundombinu, hasa katika maeneo ya vijijini: Rwanda ina daktari mmoja tu kwa kila wagonjwa 1,000, huku Shirika la Afya Duniani (WHO) likipendekeza mara nne ya idadi hiyo. Kwa kutumia teknolojia inayotegemea akili bandia (AI), programu hiyo inatumwa katika kliniki 50 kwa kipindi cha miaka miwi...

Madagascar: Kimbunga Fytia kimesababisha kifo cha mtu mmoja na zaidi ya watu 8,000 wameathiriwa

Image
  Madagascar ambayo imekumbwa na kimbunga Fytia kwa siku mbili, tangu Jumamosi Januari 31 hadi Jumapili Februari 1, sasa inajaribu kutathmini uharibifu uliosababishwa na kimbunga hicho. Ingawa uharibifu unaweza kuonekana mdogo, hasa huko Antananarivo, wakazi wa vitongoji kadhaa katika mji mkuu bado wanaishi katika mafuriko. Kimbunga Fytia kilivuka Madagascar kutoka magharibi hadi mashariki mwishoi mwa wiki hii iliyopita. Kulingana na ripoti ya hivi karibuni kutoka Ofisi ya Kitaifa ya Usimamizi wa Majanga na Maafa (BNGRC), kimunga Fytia kimesababisha mmoja kifo cha mtu mmoja, mwengine mmoja hajulikani alipo, na karibu watu 8,400 wameathiriwa. Baada ya kutua alfajiri Jumamosi, Januari 31, karibu na Majunga kaskazini-magharibi mwa kisiwa hicho, kikiambatana na upepo mkali unaofikia hadi kilomita 210 kwa saa, kimbunga hicho kilirudi baharini, kikiwa kimepunguza kasi na kuwa kimbunga cha wastani cha kitropiki, kutoka pwani ya mashariki asubuhi ya Jumapili, Februari 1. Wakati huo huo, km...

Uganda: Washington yaghadhabishwa na kauli za mkuu wa jeshi ambaye ni mtoto wa rais

Image
  Marekani lazima itathmini upya ushirikiano wake wa usalama na Uganda, Jim Rish kutoka chama cha Republican, ambaye ni mwenyekiti wa Kamati ya Mahusiano ya Kigeni ya Baraza la Seneti, ametangaza kwenye mtandao wa kijamii  wa X. Msururu wa jumbe zilizochapishwa kwenye jukwaa hilo la X na Jenerali Muhoozi Kainerugaba ambapo alishutumu ubalozi wa Marekani mjini Kampala kwa kumsaidia kiongozi wa upinzani Bobi Wine kutoroka nyumbani kwake wakati wa uvamizi wa jeshi, muda mfupi baada ya uchaguzi wa urais Januari 15. Kufuatia kuchapishwa kwenye mtandao wa kijamii wa X kwa machapisho kadhaa na mkuu wa jeshi la Uganda—ambaye pia ni mtoto wa rais Yoweri Museveni—mwenyekiti wa Kamati ya Mahusiano ya Kigeni ya Baraza la Seneti la Marekani ameghadhabishwa. Jenerali Kainerugaba amevuka mstari: Marekani sasa lazima itathmini upya ushirikiano wake wa usalama na Uganda, Jim Rish aliandika kwenye mtandao wa kijamii wa X. Sababu? Msururu wa jumbe kutoka kwa Jenerali Muhoozi Kainerugaba ulishutu...

MWIGULU NCHEMBA NDIYE WAZIRI MKUU MTEULE

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Hassan Suluhu amempendekeza aliyekuwa Waziri wa Fedha na Mbunge wa Iramba Magharibi, Mwigulu Lameck Nchemba kuwa Waziri Mkuu wa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kinachosubiriwa kwa sasa baada ya jina kuwasilishwa kwa Spika wa Bunge ni mchakato wa kuthibitishwa kwa jina hilo na bunge

Zungu Spika Mpya wa Bunge la Tanzania

Image
  Mussa Azzan Zungu amechaguliwa kuwa Spika mpya wa Bunge la 13 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Zungu alipata kura 378 kati ya kura 383 zilizopigwa na wabunge katika mkutano wa kwanza na kikao cha kwanza cha bunge la 13 la Tanzania. Kwa ushindi huo, Mussa Azzan Zungu anakuwa Spika wa nane wa Bunge hilo tangu kuanzishwa kwake, baada ya kuwashinda wagombea wa vyama vingine waliopata jumla ya kura mbili pekee. Zungu aliteuliwa na chama chake, Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuwania nafasi hiyo, huku Spika, Dk. Tulia Ackson akijitoa katika kinyang’anyiro hicho kwa sababu ambazo hazikuelezwa wazi. Zungu, atasaidiwa na Daniel Sillo ambaye ameteuliwa kuwa Naibu Spika. Miongoni mwa waliowahi kushika wadhifa huo wa Spika katika historia ya Tanzania ni Adam Sapi Mkwawa, Erasto Andrew Mbwana Mang’enya, Pius Msekwa, Samuel John Sitta, Anna Makinda, Job Ndugai, na Dk. Tulia Ackson.