Posts

MWIGULU NCHEMBA NDIYE WAZIRI MKUU MTEULE

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Hassan Suluhu amempendekeza aliyekuwa Waziri wa Fedha na Mbunge wa Iramba Magharibi, Mwigulu Lameck Nchemba kuwa Waziri Mkuu wa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kinachosubiriwa kwa sasa baada ya jina kuwasilishwa kwa Spika wa Bunge ni mchakato wa kuthibitishwa kwa jina hilo na bunge

Zungu Spika Mpya wa Bunge la Tanzania

Image
  Mussa Azzan Zungu amechaguliwa kuwa Spika mpya wa Bunge la 13 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Zungu alipata kura 378 kati ya kura 383 zilizopigwa na wabunge katika mkutano wa kwanza na kikao cha kwanza cha bunge la 13 la Tanzania. Kwa ushindi huo, Mussa Azzan Zungu anakuwa Spika wa nane wa Bunge hilo tangu kuanzishwa kwake, baada ya kuwashinda wagombea wa vyama vingine waliopata jumla ya kura mbili pekee. Zungu aliteuliwa na chama chake, Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuwania nafasi hiyo, huku Spika, Dk. Tulia Ackson akijitoa katika kinyang’anyiro hicho kwa sababu ambazo hazikuelezwa wazi. Zungu, atasaidiwa na Daniel Sillo ambaye ameteuliwa kuwa Naibu Spika. Miongoni mwa waliowahi kushika wadhifa huo wa Spika katika historia ya Tanzania ni Adam Sapi Mkwawa, Erasto Andrew Mbwana Mang’enya, Pius Msekwa, Samuel John Sitta, Anna Makinda, Job Ndugai, na Dk. Tulia Ackson.

Watu 12 wameuawa katika mlipuko wa kujitoa muhanga nje ya mahakama Pakistan

Image
  \ Takriban watu 12 wamefariki katika mlipuko uliotokea nje ya mahakama katika mji mkuu wa Pakistan Islamabad. Waziri wa Mambo ya Ndani wa Pakistan Mohsin Naqvi ameviambia vyombo vya habari kuwa watu 12 wamefariki na watu 27 wamejeruhiwa katika tukio hili. Mohsin Naqvi amesema, "Shambulio la kujitoa mhanga lilitokea mahakamani saa za jioni. Shambulio hili limesababisha uharibifu mkubwa, na watu 12 wameuawa na karibu 27 kujeruhiwa." Shirika la habari la Reuters lkimnukuu msemaji wa polisi akisema kuwa hali za baadhi ya waliojeruhiwa ni mbaya. Mlipuko huo ulitokea karibu na lango la Mahakama ya Wilaya ya Islamabad, ambayo kwa kawaida huwa na watu wengi wanaokuja mahakamani. Baada ya tukio hili, Waziri wa Ulinzi wa Pakistan Khawaja Asif amechapisha kwenye Instagram akisema kuwa Pakistan iko katika hali ya vita. Aliandika kwenye X, "Ikiwa mtu yeyote anafikiri kwamba Jeshi la Pakistan linapigana vita katika eneo la mpaka wa Afghanistan na Pakistani na maeneo ya mbali ya Balo...

Rais Samia Suluhu Hassan afanya uteuzi wa mwanasheria mkuu wa serikali mpya

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika siku yake ya kwanza ya kuanza rasmi muhula wake wa pili wa uongozi baada ya kula kiapo cha kuiongoza Tanzania, amemteua Bw. Hamza Said Johari kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kupitia mitandao ya kijamii na Msemaji wa Serikali, Bw. Gerson Msigwa, imeelezwa kuwa Bw. Hamza Said Johari ataapishwa siku ya Jumatano, tarehe 5 Novemba 2025, saa 4:00 asubuhi, katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino, Dodoma.

Kanali Mamadi Doumbouya atangaza kugombea urais Guinea licha ya ahadi ya kutowania

Image
Kanali Mamadi Doumbouya aliyenyakua madaraka Guinea kupitia mapinduzi ya kijeshi miaka minne iliyopita,atashiriki katika uchaguzi wa rais licha ya kuahidi hapo awali kuwa hatawania urais na atarejesha utawala wa kiraia. Kanali Doumbouya aliwasili katika mahakama ya juu hapo jana Jumatatu akiwa amendamana na wanajeshi kuwasilisha rasmi azma yake ya kugombea urais. Vyama viwili vikuu vya upinzani vimepigwa marufuku kushiriki katika uchaguzi huo unaotarajiwa mwezi ujao Desemba. Waguinea walishangazwa na tangazo kuwa wagombea urais watahitajika kulipa ada ya dola laki moja kushiriki katika uchaguzi huo. Mnamo Septemba mwaka 2021,mapinduzi ya kushtukiza ya kijeshi yalifanyika nchini Guinea nakumaliza hatamu yenye utata ya Rais Alpha Conde, chini ya mwaka mmoja baada ya kushinda muhula wa tatu uliogubikwa na maandamano mabaya na ukandamizaji mkali dhidi ya upinzani katika taifa hilo la magharibi mwa Afrika.

Mtandao warejea Tanzania

Image
  Hatimaye mtandao umerejea nchini Tanzania baada ya kufinywa kwa siku sita. Hili imehjiri baada ya Rais Samia kuapishwa na kuchukua majukumu yake rasmi. Katika hotuba aliyotoa wakati wa kuapishwa kwake Rais Samia alitoa maagizo kwa vyombo vya usalama kuhakikisha hali imerejea kama kawaida kwa Watanzania. "Kamati ya kitaifa na kamata za ulinzi za mikoa na wilaya nawataka muhakikishe, kuanzia leo maisha ya wananchi yanarejea mara moja," alisema Rais Samia. Kuzimwa kwa mtandao kuliathiri mawasiliano, biashara, kudorora kwa utalii mbali na hata kuwa vigumu kujua hali inavyoendelea nchini humo Tanzania.

Serikali ya Tanzania yatangaza kurejea kwa shughuli kama kawaida

Image
  Msemaji wa Serikali Gerson Msigwa ametoa ujumbe kuwajulisha wananchi kuwa shughuli za kijamii na kiuchumi zinarejea kama kawaida kuanzia kesho, Jumanne tarehe 4 Novemba 2025. "Wananchi wanaaswa kuendelea kuzingatia tahadhari ya miongozo ya kiusalama kadri itakavyokuwa inatolewa na vyombo vya Ulinzi na Usalama katika maeneo yao,"ujumbe huo umesema. Katika hotuba ya kuapishwa kwake, Rais Samia aliagiza kurejea kwa hali ya kawaida mara moja.