CEO WA SAMSANG AFARIKI
Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya teknolojia ya Korea Kusini, Samsung Electronics, Han Jong-Hee, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 63.
Han Jong-Hee alizaliwa mwaka 1962 na alijiunga na kampuni ya Samsung Electronics mwaka 1988 baada ya kumaliza Shahada yake ya Kwanza ya Uhandisi wa Umeme katika Chuo Kikuu cha Inha nchini Korea Kusini.
Tangu mwaka 2022, aliteuliwa kuwa Makamu Mwenyekiti na Mkurugenzi Mkuu wa kampuni hiyo, akisimamia maeneo ya vifaa vya kielektroniki vya nyumbani na simu za mkononi.