Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Jenerali Jacob Mkunda, kwa niaba ya Rais na Amiri Jeshi Mkuu, Samia Suluhu Hassan, amewavisha nishani mbalimbali maafisa na askari wa JWTZ jijini Mbeya leo, Machi 26, 2025. Akizungumza baada ya kuvisha nishani hizo, Jenerali Mkunda amewapongeza maafisa na askari waliotunukiwa kwa jinsi Rais Samia Suluhu Hassan alivyotambua mchango wao katika kulitumikia taifa kwenye nyanja ya ulinzi. Aidha, amewataka maafisa na askari kuendelea kuviishi viapo vyao na kuhakikisha mipaka yote ya nchi inabaki salama wakati wote. Nishani walizotunukiwa askari hao ni Nishani ya Kumbukumbu ya Muungano Daraja la Nne, Nishani ya Utumishi Uliotukuka, Nishani ya Utumishi Mrefu na Tabia Njema, Nishani ya Miaka 60 ya JWTZ, na Nishani ya Jumuiya ya SADC
Rais wa Uganda akifanya mazoezi Ikulu, nchini Uganda katika msimu wa Uviko19 / Picha: Reuters Serikali ya Uganda imeamrisha wizara, na mashirika ya umma kuanzisha mazoezi ya kila wiki. Hii, serikali imesema ni kwa ajili ya kupunguza magonjwa yanayohusiana na hali ya maisha. Mkuu wa huduma ya umma alisema haya katika barua ambayo aliandikia wizara za serikali. "Hii ni kuwaarifu ....kutenga masaa mawili kila wiki katika taasisi zenu kwa jili ya kuhimiza afya njema," barua hiyo kutoka kwa Lucy Nayobe mkuu wa huduma ya umma ilisema, " Mchukukie suala hili kwa umakini." Maagizo haya yalitolewa baada ya ripoti ya uchunguzi wa demografia na afya ya Uganda ambayo ilionyesha kuongezeka kwa unene kutoka asilimia 17 hadi 26 kati ya mwaka 2006 hadi 2022. Uzito kupita kiasi na unene unahusishwa na hatari ya magonjwa ya kawaida kama vile ugonjwa wa kisukari, moyo na saratani. Utafiti katika taasisi ya saratani ya Uganda umeonya katika ripoti ya mwaka 2022 kwamba changamoto ya sar...
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amefanya ukaguzi wa viwanja vitakavyotumiwa kufanya mazoezi na timu zitakazoshiriki michuano ya CHAN ambayo inatarajiwa kuanza kutimua vumbi mwezi Agosti mwaka huu pamoja na michuano ya AFCON 2027 ikiwa ni ushirikiano wa nchi tatu, Tanzania, Kenya na Uganda. Baada ya ukaguzi huo Waziri Mkuu, amewaagiza Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, na Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kushirikiana na Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kufanya tathmini ya kazi ya ujenzi na ukarabati wa viwanja vya mazoezi vitakavyotumika kwenye michuano hiyo. Waziri Mkuu ametoa maelekezo hayo jana Machi 29, 2025 baada ya kupokea maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa SUMA JKT, Brigedia Jenerali Petro Ngata ambao ndiyo wakandarasi wa mradi huo.