Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Jenerali Jacob Mkunda, kwa niaba ya Rais na Amiri Jeshi Mkuu, Samia Suluhu Hassan, amewavisha nishani mbalimbali maafisa na askari wa JWTZ jijini Mbeya leo, Machi 26, 2025. Akizungumza baada ya kuvisha nishani hizo, Jenerali Mkunda amewapongeza maafisa na askari waliotunukiwa kwa jinsi Rais Samia Suluhu Hassan alivyotambua mchango wao katika kulitumikia taifa kwenye nyanja ya ulinzi. Aidha, amewataka maafisa na askari kuendelea kuviishi viapo vyao na kuhakikisha mipaka yote ya nchi inabaki salama wakati wote. Nishani walizotunukiwa askari hao ni Nishani ya Kumbukumbu ya Muungano Daraja la Nne, Nishani ya Utumishi Uliotukuka, Nishani ya Utumishi Mrefu na Tabia Njema, Nishani ya Miaka 60 ya JWTZ, na Nishani ya Jumuiya ya SADC
Wizara ya Afya imetoa taarifa yake ambapo imeonyesha ongezeko la watu wenye maambukizi ya ugonjwa wa Uviko-19 nchini katika kipindi cha mwezi Februari hadi Aprili mwaka huu. Takwimu hizo zimetolewa leo Jumanne Mei 20, 2025, na Ofisi ya Mganga Mkuu wa Serikali, Dk. Grace Magembe kupitia taarifa yake kwa umma, ambapo amesema kumekuwepo ongezeko la tetesi zinazohusiana na magonjwa ya mfumo wa njia ya hewa katika jamii nchini. “Hali ya kuongezeka na kupungua kwa ugonjwa huu imekuwepo kila mwaka tangu kutangazwa kwa ugonjwa huu mwaka 2020. Kwa kipindi hiki ongezeko hili linaonekana zaidi katika Mkoa wa Dar es Salaam,” amesema Dk. Magembe. Dk. Magembe amesema kupitia mfumo wa ufuatiliaji wa magonjwa ya mfumo njia ya hewa, wizara imebaini kuna ongezeko la wagonjwa wenye Uviko-19 kutoka wawili kati ya watu 139 waliopimwa Februari sawa na asilimia 1.4 hadi wagonjwa 31 kati ya watu 185 waliopimwa Aprili mwaka huu, sawa na asilimia 16.8. “Tangu Februari hadi Aprili 2025, ufuatiliaji wa viru...
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amefanya ukaguzi wa viwanja vitakavyotumiwa kufanya mazoezi na timu zitakazoshiriki michuano ya CHAN ambayo inatarajiwa kuanza kutimua vumbi mwezi Agosti mwaka huu pamoja na michuano ya AFCON 2027 ikiwa ni ushirikiano wa nchi tatu, Tanzania, Kenya na Uganda. Baada ya ukaguzi huo Waziri Mkuu, amewaagiza Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, na Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kushirikiana na Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kufanya tathmini ya kazi ya ujenzi na ukarabati wa viwanja vya mazoezi vitakavyotumika kwenye michuano hiyo. Waziri Mkuu ametoa maelekezo hayo jana Machi 29, 2025 baada ya kupokea maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa SUMA JKT, Brigedia Jenerali Petro Ngata ambao ndiyo wakandarasi wa mradi huo.