Wawakilishi wa Marekani leo wanatarajiwa kufanya mazungumzo na wenzao wa Iran huko Muscat, Oman kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran. Upande wa Marekani, mjumbe maalum Steve Witkoff na Jared Kushner, mkwe wa Rais Donald Trump, watashiriki. Ajenda halisi ya mkutano huo bado haijulikani. Wizara ya mambo ya nje ya Iran imesema Iran inapania kuyawekea mipaka mazungumzo hayo yajikite katika mpango wa nyuklia wa Iran na kulegezwa kwa vikwazo. Marekani ingependa kuongeza mada zaidi kwenye ajenda, ikiwa ni pamoja na mpango wa makombora wa Iran na msaada kwa washirika wake, ikiwa ni pamoja na kundi la Hamas katika Ukanda wa Gaza, wanamgambo wa Hezbollah nchini Lebanon na waasi wa Houthi nchini Yemen.
Madagascar ambayo imekumbwa na kimbunga Fytia kwa siku mbili, tangu Jumamosi Januari 31 hadi Jumapili Februari 1, sasa inajaribu kutathmini uharibifu uliosababishwa na kimbunga hicho. Ingawa uharibifu unaweza kuonekana mdogo, hasa huko Antananarivo, wakazi wa vitongoji kadhaa katika mji mkuu bado wanaishi katika mafuriko. Kimbunga Fytia kilivuka Madagascar kutoka magharibi hadi mashariki mwishoi mwa wiki hii iliyopita. Kulingana na ripoti ya hivi karibuni kutoka Ofisi ya Kitaifa ya Usimamizi wa Majanga na Maafa (BNGRC), kimunga Fytia kimesababisha mmoja kifo cha mtu mmoja, mwengine mmoja hajulikani alipo, na karibu watu 8,400 wameathiriwa. Baada ya kutua alfajiri Jumamosi, Januari 31, karibu na Majunga kaskazini-magharibi mwa kisiwa hicho, kikiambatana na upepo mkali unaofikia hadi kilomita 210 kwa saa, kimbunga hicho kilirudi baharini, kikiwa kimepunguza kasi na kuwa kimbunga cha wastani cha kitropiki, kutoka pwani ya mashariki asubuhi ya Jumapili, Februari 1. Wakati huo huo, km...