Watu 25 wameuawa katika mashambulio mawili ya kijihadi katika jimbo la Adamawa, Kaskazini Mashariki mwa Nigeria. Ripoti zinasema, mashambulio hayo yalitokea katika miji miwili ya Madagali na Hong inayopakana na Cameroon. Wanajihadi wa Boko Haram wanadaiwa kuhusika na mashambulio hayo kwa sababu wamekuwa wakidhibiti eneo hilo tangu mwaka 2009. Watu wenye silaha waliokuwa kwenye pikipiki walivamia soko katika mji wa Madagali na kuwauwa watu 21 papo hapo, huku idadi hiyo ikitarajiwa kuongzeka kwa sababu wenyeji wanasema watu wengine hawajapatikana. Mbali na mauaji hayo, watu hao wenye silaha, wameiba vyakula na pikipiki zilizokuwa kwenye soko hilo, huku watu wengine wanne wakipoteza maisha kwenye mji jirani wa Hong. Katika hatua nyingine, wanajihadi kutoka kundi la Lakurawa, wamewauwa waumini watano na kuwajeruhi wengine watatu, baada ya kushambuliwa kwa msikiti, katika jimbo la Kebbi, Kaskazini Magharibi mwa Nigeria.
Mradi huoI ambao unaitwa Horizon 1000, uliotengenezwa na Wakfu wa Gates na kampuni ya Marekani ya OpenAI kwa ushirikiano na mamlaka ya Rwanda, unalenga kushughulikia uhaba mkubwa wa wataalamu wa afya nchini. Ikiwa imejaribiwa kwa miaka miwili katika kliniki zipatazo hamsini za Rwanda, programu hiyo inaweza kutumwa katika vituo 1,000 vya afya kote barani Afrika ikiwa matokeo yatakuwa ya uhakika. Je, akili bandia (AI) inaweza kuboresha upatikanaji na ubora wa huduma za afya? Nchini Rwanda, Wakfu wa Gates kwa sasa unazindua programu ya majaribio ya programu mpya iliyoundwa ili kuwasaidia wataalamu wa afya katika kufanya maamuzi yao. Nchi hii inakabiliwa na uhaba mkubwa wa wafanyakazi wa afya na miundombinu, hasa katika maeneo ya vijijini: Rwanda ina daktari mmoja tu kwa kila wagonjwa 1,000, huku Shirika la Afya Duniani (WHO) likipendekeza mara nne ya idadi hiyo. Kwa kutumia teknolojia inayotegemea akili bandia (AI), programu hiyo inatumwa katika kliniki 50 kwa kipindi cha miaka miwi...