Mtandao warejea Tanzania

 


Hatimaye mtandao umerejea nchini Tanzania baada ya kufinywa kwa siku sita.


Hili imehjiri baada ya Rais Samia kuapishwa na kuchukua majukumu yake rasmi.

Katika hotuba aliyotoa wakati wa kuapishwa kwake Rais Samia alitoa maagizo kwa vyombo vya usalama kuhakikisha hali imerejea kama kawaida kwa Watanzania.

"Kamati ya kitaifa na kamata za ulinzi za mikoa na wilaya nawataka muhakikishe, kuanzia leo maisha ya wananchi yanarejea mara moja," alisema Rais Samia.

Kuzimwa kwa mtandao kuliathiri mawasiliano, biashara, kudorora kwa utalii mbali na hata kuwa vigumu kujua hali inavyoendelea nchini humo Tanzania.

Habari Zilizotrendi:

Watumishi wa umma Uganda washurutishwa kufanya mazoezi kila wiki

Kutoka gerezani hadi urais: Hadithi ya Bassirou Faye wa Senegal

Wagonjwa wa Uviko-19 Waongezeka