Watu 12 wameuawa katika mlipuko wa kujitoa muhanga nje ya mahakama Pakistan
Takriban watu 12 wamefariki katika mlipuko uliotokea nje ya mahakama katika mji mkuu wa Pakistan Islamabad.
Waziri wa Mambo ya Ndani wa Pakistan Mohsin Naqvi ameviambia vyombo vya habari kuwa watu 12 wamefariki na watu 27 wamejeruhiwa katika tukio hili.
Mohsin Naqvi amesema, "Shambulio la kujitoa mhanga lilitokea mahakamani saa za jioni. Shambulio hili limesababisha uharibifu mkubwa, na watu 12 wameuawa na karibu 27 kujeruhiwa."
Shirika la habari la Reuters lkimnukuu msemaji wa polisi akisema kuwa hali za baadhi ya waliojeruhiwa ni mbaya.
Mlipuko huo ulitokea karibu na lango la Mahakama ya Wilaya ya Islamabad, ambayo kwa kawaida huwa na watu wengi wanaokuja mahakamani.
Baada ya tukio hili, Waziri wa Ulinzi wa Pakistan Khawaja Asif amechapisha kwenye Instagram akisema kuwa Pakistan iko katika hali ya vita.
Aliandika kwenye X, "Ikiwa mtu yeyote anafikiri kwamba Jeshi la Pakistan linapigana vita katika eneo la mpaka wa Afghanistan na Pakistani na maeneo ya mbali ya Balochistan, basi shambulio la leo la kujitoa mhanga katika Mahakama ya Wilaya ya Islamabad ni wito kwamba hivi ni vita kwa Pakistan yote."